Afrika
1 dk kusoma
Rais wa Kenya atoa salamu za Ramadhan
Ramadhan ya mwaka huu inatarajiwa kuanza Machi 1 na kukamilika Machi 30. Mwezi huo wa mfungo unafikia mwisho kwa kusherehekea sikukuu ya Eid al-Fitr, ambapo Waislamu hujumuika pamoja katika ibada.
Rais wa Kenya atoa salamu za Ramadhan
Rais William Ruto ameomba Waislamu waiombee Kenya wanapoanza mwezi mtukufu wa Ramadhan /Picha kutoka Rais Willim Ruto kwa X
tokea masaa 5

Rais wa Kenya William Ruto ametoa ujumbe maalum kuwatakia heri Waislamu kote nchini wanapojiandaa kuanza kufunga katika mwezi mtukufu wa Ramadhan.

“ Tunakumbushwa thamani na umuhimu wa kipindi hiki takatifu. Ramadhan sio tu mwezi wa kujizuia na starehe bali ni wakati wa ibada, sadaka, ukarimu na tafakari ya kina,” Rais Ruto ameongezea.

Amewakumbusha Waislamu kwamba huu ulikuwa wakati muhimu wa kutafakari kiimani, nidhamu binafsi, na kujitolea kufanya hisani zaidi.

“Ni fursa adhimu ya kila mmoja kujitakasa nafsi, kuimarisha imani na kujitolea katika matendo ya haki.” amesema.

“ Mnapoanza safari hii ya kiroho nawahimiza muombee nchi yetu na raia wake. Muwafikirie na kuwasaidia wale wasiojiweza. Na mdumishe maadili ya huruma mshikamano wa kujitolea kwa ajili ya wenzenu,” Rais Ruto amesema akiwatakia Waislamu Ramadhan Mubarak.

Tazama TRT Global. Shiriki maoni yako!
Contact us