Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) imewateua viongozi wa zamani Uhuru Kenyatta kutoka Kenya, Olusegun Obasanjo kutoka Nigeria, na Hailemariam Desalegn kutoka Ethiopia kuwa wawezeshaji wa mpango wa pamoja wa amani unaolenga kutatua mzozo Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Uamuzi huo ulifikiwa wakati wa Mkutano wa ngazi ya juu wa Pamoja wa Wakuu uliofanyika jijini Dar es Salaam Februari 8, 2025, ulioongozwa na Rais wa Zimbabwe na Mwenyekiti wa SADC Emmerson Mnangagwa na Rais wa Kenya na Mwenyekiti wa EAC William Ruto.
Mkutano huo ulilenga kuimarisha juhudi za kikanda za kurejesha utulivu mashariki mwa DRC, ambayo imekuwa ikikumbwa na migogoro ya kivita inayoendelea.
Katika taarifa iliyochapishwa katika mtandao wa X, Rais William Ruto alisme Hatua hii inatarajiwa kuongeza juhudi za kidiplomasia, kuhakikisha jibu la ufanisi zaidi kwa mgogoro unaoendelea.